WANANCHI WAKOMBOLEWA KWA MRADI WA MAJI WA MILIONI 292


Mbunge wa Jimbo la Kondoa ambae pia ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amefanya uzinduzi wa mradi wa maji uliogarimu kiasi cha shilingi million 292 katika kijiji cha kwadelo kilichopo Wilaya ya Kondoa kata ya kwadelo, ulio tekelezwa na kampuni ya Serengeti Breweries
Katika uzinduzi huo Waziri Ashatu amesema mradi huu wa maji umetatua changamoto kubwa ya maji iliokua ikiwasubumbua wananchi na kuhatarisha maisha yao kwakufwata maji umbali mrefu hususani wanawake.

Pia Katika hotuba yake Waziri Ashatu amewataka wananchi kuutunza mradi huo na nijukumu la kila mtu kuutuza kuanzia kwenye vyanzo vya maji ili uzidi kusaidia kizazi cha sasa na vijavyo.

Aidha ameitaka kampuni ya Serengeti breweries kuendelea kuwa saidia wananchi wa kondoa kwa kuwa ongezea mradi mwingine wa maji ambao utasaidia kutatua chanagmoto ya maji kati baadhi ya maeneo yalio baki
Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Serengeti breweries Dkt. Obinna Anyalebechi amewashukuru wanachi wa kwadelo kwa ushirikiano mkubwa walio utoa katika kukamilisha mradi huu na amewataka kushirikiana kuutunza mradi huo kwa manufaa yao na kijiji.
Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Dodoma Bw. Mbaraka Rajabu amesema lengo la serikali kupitia Ruwasa ni kuhakikisha uboreshaji wa miundombinu ya maji na kuhakikisha wananchi wote wanapa huduma ya maji kwa uraisi


