PABLO GAVI ATUA MAPUMZIKONI HIFADHI YA SERENGETI

0
499042971_18511641532053708_7325755086741287943_n

Nyota wa Barcelona na timu ya Taifa ya Hispania, Pablo Gavi amefuata nyayo za baadhi ya mastaa wa soka wa nchi yake kwa kuja mapumzikoni Tanzania.

Kiungo huyo yupo katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti sambamba na mpenzi wake, Ana Pelayo.

Gavi ametua Tanzania ikiwa ni siku chache baada ya nyota wengine watatu wa soka wa Hispania kutembelea hapa nchini kwa ajili ya mapumziko.

Wachezaji hao ni David Raya, David De Gea na Pedri.

Ukiondoa Wahispania hao, pia Tanzania imepokea nyota wengine wawili wa soka ambao ni mshambuliaji mstaafu wa Sweden, Barcelona na AC Milan, Zlatan Ibrahimovic na mshambuliaji wa Girona na Uholanzi, Arnaut Danjuma.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *