DKT. ASHATU- WAFUGAJI KUUPOKEA UFUGAJI WA KISASA

0
IMG-20250615-WA0017

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amesema kuwa wafugaji wameonyesha nia kuupokea ufugaji wa kisasa ili kuongeza tija kwenye sekta ya mifugo nchini.

Mhe. Dkt. Kijaji amesema hayo leo (Juni 15, 2025) wakati wa Kongamano la Wafugaji Tanzania lililofanyika katika Viwanja vya Nanenane Nyakabindi vilivyopo Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu.

“Tupo tayari kubadilika na kuanza kufuga kisasa kwa kutumia njia za kisasa ili kufikia mageuzi makubwa ya serikali kwenye Sekta ya Mifugo nchini” amesema Mhe. Dkt. Kijaji

Aidha, amesema wizara imefanya mikutano na wafugaji wote nchini kwa kukutana na wawakilishi wao ili kujadili changamoto za sekta hiyo na kuzigeuza kuwa fursa ili kuiboresha Sekta ya Mifugo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *