SERIKALI ITAENDELEA KUIPA KIPAUMBELE TMA – WAZIRI MWIGULU

0

Waziri wa Fedha, Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba ameipongeza Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na kuahidi kuwa Serikali kupitia Wizara ya Fedha itaendelea kuipa kipaumbele kwa kuwa huduma za hali ya hewa zinasaidia katika mipango mbalimbali ya maendeleo.

“Wataalam wa hali ya hewa mnafanya kazi nzuri, utabiri unaotolewa hivi sasa ni wa usahihi na umesaidia sana katika masuala ya kiuchumi na kijamii na mipango ya nchi kwa ujumla”.

Dkt. Mwigulu ameyasema hayo wakati alipotembelea banda la TMA katika Viwanja vya AICC, Arusha wakati akifunga rasmi Jukwaa la 16 la Ununuzi la Afrika Mashariki.

Matumizi sahihi ya huduma za hali ya hewa ni suala mtambuka kwani husaidia katika mipango na uendeshaji wa shughuli za kiuchumi na kijamiii hususani katika kupunguza madhara yatokanayo na hali mbaya ya hewa kwa umma.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *