UENDELEZAJI WA MRADI WA KABANGA NICKEL WAUNGWA MKONO NA WADAU MBALIMBALI KIMATAIFA

0

Dar es salaam

Serikali ya Marekani yasisitiza nia ya kushiriki katika kuendeleza Mradi wa Kabanga Nickel na Kampuni ya BHP imeweka mkazo wa ushiriki wake katika Mradi huo ambao ni kati ya miradi mikubwa na kielelezo katika sekta ya madini nchini ambapo utekelezaji wa Mradi huu wa Madini Mkakati ni muhimu kwa wakati huu ambapo madini haya yanayohitajika sana duniani hususani kwa ajili ya mageuzi ya nishati.

Hayo yamesemwa jana katika mazungumzo kati ya Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde na kampuni ya Tembo Nickel ambayo Serikali ya Tanzania ni Mbia ili kupokea ujumbe maalum kutoka kwa Kampuni mama ya Tembo Nickel pamoja na Serikali ya Marekani kupitia kwa Balozi wa Marekani nchini Tanzania Balozi Battle na
Ujumbe wa Marekani uliobebwa na Bi.Helaina Matza, Mratibu Maalum wa Idara ya Mambo ya Nje ya Marekani kwa Ajili ya Mpango maalum wa Nchi Saba Zilizoendelea Zaidi Kiuchumi Duniani G7.

Katika ujumbe huo uliowasilishwa ma Bi. Matza umebeba malengo ya kuwezesha miradi mbalimbali ya kimkakati (PGII) na pia unathibitisha kuwa nchi ya Tanzania ni nchi inayovutia wawekezaji na mazingira ya uwekezaji ni rafiki na hii imechochewa sana falasafa ya uongozi wa Mh Rais Dkt.Samia S. Hassan ya 4R-Reconciliation (Maridhiano), Resilience (Ustahimilivu), Reform (Mabadiliko) na Rebuilding (Kujenga upya).

Akizungumza katika mkutano huo Waziri Mavunde ametoa shukrani kwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuimarisha zaidi uhusiano na Marekani ambao ndio umeleta mafanikio haya.

Mafanikio haya yanatokana na mikakati ya Mh. Rais katika mashauriano yake kwenye Mkutano wa Marekani na Afrika uliofanyika mwaka 2022 na pia ujio wa Makamu wa Rais wa Marekani Kamala Harris wakati wa ziara yake Tanzania mwezi Machi 2023.

Waziri Mavunde alipata wasaa wa kukutana na Afisa Mkuu wa Maendelezo wa Kampuni ya BHP Bi. Catherine Raw aliyekuja nchini kutizama maendeleo ya Mradi wa Kabanga Nickel na kuisisitizia Serikali ya Tanzania nia ya kushiriki katika kuendelea Mradi huu ambao unaenda sambamba na ujenzi wa kiwanda kikubwa cha kusafisha madini kitakachojengwa Wilayani Kahama,Mkoa wa Shinyanga uwekezaji utakaogharimu zaidi ya Dola Milioni 500.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *