MAMA SAMIA KAITEKA MOROGORO NA KUKONGA MOYO TAIFA

0

Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ameendelea na ziara yake ya kikazi mkoani Morogoro, akithibitisha tena dhamira yake ya dhati ya kuleta maendeleo ya haraka na kuimarisha maisha ya wananchi. Wakati wapinzani wakiendelea na malalamiko yasiyo na msingi, Rais Samia anajenga Tanzania ya kesho kwa vitendo.

Elimu:
Rais Samia ameondoa gharama za wazazi kusomesha watoto, hatua ambayo imewapa watoto wa Kilombero nafasi ya kusoma bila vikwazo. Shule za msingi 184 sasa zinaendeshwa bila mzigo kwa wazazi, akiwahimiza waache watoto wao wasome kwani wao ndio kesho ya Tanzania. Katika ziara yake, Rais Samia amekemea vikali watoto kuzurura mitaani badala ya kuwa shule, akionesha jinsi anavyothamini elimu.

Maendeleo ya Wakulima:
Chini ya uongozi wake, Wakala wa Uhifadhi wa Chakula (NFRA) sasa wananunua mpunga kwa bei ya TZS 900 kutoka TZS 570. Ongezeko hili limeleta tija kwa wakulima wa bonde la Kilombero, ikiwapa motisha zaidi ya kuzalisha kwa wingi.

Ujenzi wa Miundombinu:
Rais Samia ameendelea kuimarisha sekta ya miundombinu kwa kufungua barabara ya Rudewa-Kilosa yenye urefu wa kilomita 25, hatua itakayorahisisha usafiri na usafirishaji wa bidhaa. Pia, ameweka jiwe la msingi kwa ujenzi wa kiwanda cha sukari cha Kilombero (K4) ambacho kitaleta ajira nyingi na kuongeza uzalishaji wa sukari nchini, kupunguza utegemezi wa uagizaji kutoka nje.

Ajira na Uchumi:
Rais Samia anaposema ajira ni kipaumbele, anamaanisha na kutenda. Ameagiza waziri mpya wa vijana, kazi na ajira kuandaa ripoti ya ni ajira ngapi mpya zitakua zimeanzishwa ifikapo mwisho wa mwaka huu, akionesha dhamira ya dhati ya kuimarisha uchumi wa nchi na kuongeza ajira kwa vijana.

Upatikanaji wa Umeme:
Katika juhudi za kuboresha upatikanaji wa umeme, Rais Samia ametembelea na kukagua kituo cha kupoza umeme cha Ifakara, kuhakikisha umeme wa uhakika unapatikana kwa wananchi wa Morogoro na maeneo mengine. Hii ni hatua muhimu kwa maendeleo ya viwanda na ustawi wa jamii kwa ujumla.

Ukaribu na Wananchi:
Rais Samia ameonyesha ukaribu wake na wananchi kwa kuwasalimia katika round about ya Mikumi, hatua inayoonyesha anavyothamini mawazo na hisia za wananchi wake, kujenga mazingira ya uwazi na ushirikiano.

Jengo Mtambuka la Mafunzo – SUA:
Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amezindua jengo Mtambuka la Mafunzo katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kwenye Kampasi ya Edward Moringe, mkoani Morogoro tarehe 06 Agosti, 2024. Jengo hili jipya litaboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia, likitoa nafasi kwa wanafunzi wa kilimo kupata maarifa ya kisasa na teknolojia za kilimo, hivyo kuchangia katika kuboresha sekta ya kilimo nchini.

Kiwanda cha Sigara cha Serengeti (SCC):
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amezungumza na viongozi mbalimbali mara baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Kiwanda cha Sigara cha Serengeti (SCC) katika eneo la Kiwanda cha uchakataji tumbaku Mkwawa (MTPL) mkoani Morogoro. Kiwanda hiki kipya kitasaidia kuongeza thamani ya zao la tumbaku na kutoa ajira kwa wakazi wa Morogoro, kuchangia katika ukuaji wa uchumi wa mkoa na nchi kwa ujumla.

Manufaa kwa Wakazi wa Morogoro na Taifa kwa Ujumla:
Ziara ya Rais Samia mkoani Morogoro imeleta faida kubwa kwa wakazi wa Morogoro na nchi kwa ujumla. Miradi aliyozindua na kukagua imeimarisha miundombinu, kuleta ajira, na kuboresha huduma za kijamii kama vile elimu na upatikanaji wa umeme. Wakazi wa Morogoro wamefaidika kwa kupata miundombinu bora ya barabara, shule bora za msingi, na viwanda vipya vinavyoongeza ajira na kuimarisha uchumi wa eneo hilo.

Kwa ujumla, ziara ya Rais Samia imeleta mwanga mpya wa matumaini na maendeleo kwa wananchi wa Morogoro na taifa kwa ujumla. Imeongeza imani ya wananchi kwa serikali na kuonyesha jinsi serikali inavyofanya kazi kwa bidii kutatua changamoto zinazowakabili.

Kujitahidi Licha ya Vikwazo vya Upinzani:
Licha ya vikwazo na njama za upinzani kujaribu kuzorotesha juhudi zake, Rais Samia ameendelea kutekeleza miradi ya maendeleo kwa ufanisi mkubwa. Wapinzani wamejaribu kusababisha migogoro na kuzusha ajenda zisizo na mashiko, lakini Rais Samia ameendelea mbele kwa uthabiti, akitekeleza ahadi zake na kuleta maendeleo kwa Watanzania wote.

Rais Samia ameonyesha kuwa yeye ni kiongozi anayeweza kutimiza ahadi zake, tofauti na wapinzani wanaopoteza muda kwa kukosoa na kutafuta umaarufu kwenye mitandao ya kijamii. Rais Samia anaishi kaulimbiu yake ya Kazi Iendelee. Nasi tutaendelea kumfuatilia Mama Samia na kuona mapya anayotuletea Watanzania.

Ana Ahidi. Ana Tekeleza. Kazi Iendelee! Maneno Kidogo, Vitendo Vingi!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *