ENG. MKAMA BWIRE ATEULIWA KUWA MTENDAJI MKUU MPYA DAWASA

0

Mhandisi Mkama Bwire ameteuliwa kushika nafasi ya Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) katika kikao maalum cha Waziri wa Maji na Bodi ya Wakurugenzi DAWASA kilichofanyika leo tarehe 03 Julai, 2024 ofisi za DAWASA Jijini Dar es Salaam.

Mhandisi Bwire ni Mtumishi wa Wizara ya Maji ambae amehudumu kama Mhandisi wa Maji katika Halmashauri ya Kibaha, Mkurugenzi Mtendaji Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Tabora (TUWASA) na hadi anapokea jukumu hili alikua ni Mkurugenzi wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini katika  Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA).

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *