KAMATI YA MIUNDOMBINU YAWASILI SINGIDA KUKAGUA MIRADI YA SEKTA YA UJENZI

0

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu ikiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe.Selemani Kakoso (Mb) imewasili wilayani Itigi Mkoani Singida na kupokelewa na Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, leo tarehe 12 Machi 2024.

Kamati hiyo ikiwa Wilayani hapo itakagua na kutembelea miradi ya sekta ya ujenzi ikiwa ni pamoja na mradi wa ujenzi wa barabara ya Noranga – Itigi km 25, Barabara ya Doroto – Noranga km 6 na barabara ya Itigi – Mkiwa Km 25.57

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *